John 12:12-16
12 aSiku iliyofuata umati mkubwa uliokuwa umekuja kwenye Sikukuu walisikia kwamba Isa angekuja Yerusalemu. 13 bBasi wakachukua matawi ya mitende, wakatoka kwenda kumlaki, huku wakipaza sauti wakisema, “Hosana!” ▼▼ Kiebrania kusema Okoa, basi likawa neno la shangwe.
“Amebarikiwa yeye ajaye kwa Jina la Bwana!”
“Amebarikiwa Mfalme wa Israeli!”
14 dIsa akamkuta mwana-punda akampanda, kama ilivyoandikwa,
15 e“Usiogope, Ewe binti Sayuni;
tazama, Mfalme wako anakuja,
amepanda mwana-punda!”
16 fWanafunzi wake Isa mwanzoni hawakuelewa mambo haya, lakini Isa alipotukuzwa, ndipo walipokumbuka kuwa mambo haya yalikuwa yameandikwa kwa ajili yake na alitendewa yeye.
Copyright information for
SwhKC